Zaburi 119:145-149
145
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
146
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
147
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
148
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
149
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
Settings