Zaburi 119:113-117
113
Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
114
Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
115
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
116
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
117
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.
Settings