Skip to content
Zaburi 116:1-6

Zaburi 116:1-6

1
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
2
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
3
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni.
4
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
5
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options