Zaburi 115:12-18
12
Bwana anatukumbuka na atatubariki: ataibariki nyumba ya Israeli, ataibariki nyumba ya Aroni,
13
atawabariki wale wanaomcha Bwana, wadogo kwa wakubwa.
14
Bwana na awawezeshe kuongezeka, ninyi na watoto wenu.
15
Mbarikiwe na Bwana Muumba wa mbingu na dunia.
16
Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana, lakini dunia amempa mwanadamu.
17
Sio wafu wanaomsifu Bwana, wale washukao mahali pa kimya,
18
bali ni sisi tunaomtukuza Bwana, sasa na hata milele. Msifuni Bwana.
Settings