Skip to content
Zaburi 115:9-18

Zaburi 115:9-18

9
Ee nyumba ya Israeli, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
10
Ee nyumba ya Aroni, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
11
Ninyi mnaomcha, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
12
Bwana anatukumbuka na atatubariki: ataibariki nyumba ya Israeli, ataibariki nyumba ya Aroni,
13
atawabariki wale wanaomcha Bwana, wadogo kwa wakubwa.
14
Bwana na awawezeshe kuongezeka, ninyi na watoto wenu.
15
Mbarikiwe na Bwana Muumba wa mbingu na dunia.
16
Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana, lakini dunia amempa mwanadamu.
17
Sio wafu wanaomsifu Bwana, wale washukao mahali pa kimya,
18
bali ni sisi tunaomtukuza Bwana, sasa na hata milele. Msifuni Bwana.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options