Zaburi 112:1-4
1
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
Settings