Zaburi 111:10
Inaonyesha mstari 10 pamoja na muktadha unaouzunguka.
7
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
Settings