Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.