Skip to content
Zaburi 109:6-15

Zaburi 109:6-15

6
Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
7
Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
8
Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
9
Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
10
Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
11
Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
12
Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
13
Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
14
Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
15
Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options