Zaburi 109:21-24
21
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
22
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
24
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
Settings