Skip to content
Zaburi 108:1-5

Zaburi 108:1-5

1
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options