Skip to content
Zaburi 107:1-9

Zaburi 107:1-9

1
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options