Rukia maudhui
Zaburi 106:6-12

Dhambi za Baba Zetu: Bahari ya Shamu

Zaburi 106:6-12
6
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options