Zaburi 106:36-39
36
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Settings