Zaburi 105:39-45
39
Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
40
Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41
Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
42
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu, aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43
Aliwatoa watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za shangwe,
44
akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
45
alifanya haya ili wayashike mausia yake na kuzitii sheria zake. Msifuni Bwana.
Settings