Zaburi 105:37-41
37
Akawatoa Israeli katika nchi wakiwa na fedha na dhahabu nyingi, wala hakuna hata mmoja kutoka kabila zao aliyejikwaa.
38
Misri ilifurahi walipoondoka, kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
39
Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
40
Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41
Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
Settings