Skip to content
Zaburi 102:1-5

Zaburi 102:1-5

1
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2
Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
3
Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4
Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
5
Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options