Zaburi 102:1-11
1
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2
Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
3
Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4
Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
5
Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
6
Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
7
Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
8
Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
9
Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10
kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
11
Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
Settings