Lumaktaw sa nilalaman
Mithali 6:12-19

Mithali 6:12-19

12
Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
13
ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
14
ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
15
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
16
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
17
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
18
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
19
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options