Skip to content
Mithali 5:3-11

Mithali 5:3-11

3
Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
4
lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.
5
Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.
6
Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima; njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
7
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; msiache ninalowaambia.
8
Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
9
usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,
10
wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.
11
Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options