Mithali 3:1-6
1
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
Settings