Mithali 3:1-3
1
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.