Mithali 23:1-8
1
Uketipo kula chakula na mtawala, angalia vyema kile kilicho mbele yako,
2
na utie kisu kooni mwako kama ukiwa mlafi.
3
Usitamani vyakula vyake vitamu kwa kuwa chakula hicho ni cha hila.
4
Usijitaabishe ili kuupata utajiri, uwe na hekima kuonyesha kujizuia.
5
Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka, huwa kama umepata mabawa ghafula, ukaruka na kutoweka angani kama tai.
6
Usile chakula cha mtu mchoyo, usitamani vyakula vyake vitamu,
7
kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.
8
Utatapika kile kidogo ulichokula, nawe utakuwa umepoteza bure maneno yako ya kumsifu.
Settings