Mithali 22:12-16
12
Macho ya Bwana hulinda maarifa, bali huyapinga maneno ya asiye mwaminifu.
13
Mvivu husema, “Yuko simba nje!” au, “Nitauawa katika mitaa!”
14
Kinywa cha mwanamke kahaba ni shimo refu; yeye aliye chini ya ghadhabu ya Bwana atatumbukia ndani yake.
15
Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto, bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye.
16
Yeye amwoneaye maskini ili kujiongezea mali, naye ampaye tajiri zawadi, wote huwa maskini.
Settings