Mithali 20:20-25
20
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
21
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
22
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
23
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
24
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
25
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
Settings