Mithali 15:1-4
1
Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.
2
Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.
3
Macho ya Bwana yako kila mahali, yakiwaangalia waovu na wema.
4
Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima, bali ulimi udanganyao huponda roho.