Skip to content
Mithali 14:20-25

Mithali 14:20-25

20
Maskini huepukwa hata na majirani zao, bali matajiri wana marafiki wengi.
21
Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi, bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.
22
Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki? Bali wale wanaopanga kilicho chema hupata upendo na uaminifu.
23
Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida, bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.
24
Utajiri wa wenye hekima ni taji yao, bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.
25
Shahidi wa kweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options