Mithali 14:15-19
15
Mtu mjinga huamini kila kitu, bali mwenye busara hufikiria hatua zake.
16
Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya, bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.
17
Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu, naye mtu wa hila huchukiwa.
18
Mjinga hurithi upumbavu, bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.
19
Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema, nao waovu kwenye malango ya wenye haki.
Settings