Skip to content
Mithali 11:22-26

Mithali 11:22-26

22
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options