Mithali 1:7
Inaonyesha mstari 7 pamoja na muktadha unaouzunguka.
4
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
5
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
6
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
7
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
8
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
9
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
10
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
Settings