Skip to content
Mithali 1:7

Mithali 1:7

Inaonyesha mstari 7 pamoja na muktadha unaouzunguka.
4
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
5
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
6
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
7
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
8
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
9
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
10
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options