Mithali 1:8-19
8
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
9
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
10
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
11
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
12
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.
13
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
14
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
15
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
16
kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni wepesi kumwaga damu.
17
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu wakati ndege wote wanakuona!
18
Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!
19
Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila; huuondoa uhai wa wale wenye mali.
Settings