Skip to content
Mithali 1:24-33

Mithali 1:24-33

24
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
25
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
26
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
28
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
29
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
31
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
32
Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua, nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
33
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options