Skip to content
Mithali 1:20-31

Mithali 1:20-31

20
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
21
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
22
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
23
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
24
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
25
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
26
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
28
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
29
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
31
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options