Filemoni 1:21-25
21
Nikiwa na hakika ya utii wako, nakuandikia, nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya yale ninayokuomba.
22
Jambo moja zaidi: Niandalie chumba cha wageni, kwa kuwa nataraji kurudishwa kwenu kama jibu la maombi yenu.
23
Epafra, aliye mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu, anakusalimu.
24
Vivyo hivyo Marko, Aristarko, Dema na Luka, watendakazi wenzangu wanakusalimu.
25
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
Settings