Rukia maudhui
Hesabu 23:27-30

Maandalizi ya Unabii wa Tatu

Hesabu 23:27-30
27
Basi Balaki akamwambia Balaamu, “Njoo, nikupeleke mahali pengine. Huenda itampendeza Mungu kukuruhusu unilaanie hao watu kutoka mahali hapo.”
28
Balaki akamchukua Balaamu juu ya Mlima Peori, unaotazamana na nyika.
29
Balaamu akasema, “Nijengee hapa madhabahu saba, uandae mafahali saba na kondoo dume saba kwa ajili yangu.”
30
Balaki akafanya kama Balaamu alivyosema, kisha akatoa sadaka ya fahali mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options