Skip to content
Mathayo 7:7-11

Mathayo 7:7-11

7
“Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
8
Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
9
“Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
10
Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
11
Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options