Mathayo 6:9-13
9
“Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba: “ ‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
10
Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
11
Utupatie riziki yetu ya kila siku.
12
Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.
13
Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa Ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen].’
Settings