Mathayo 5:2
Inaonyesha mstari 2 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Basi Yesu alipoona makutano, alipanda mlimani akaketi chini, nao wanafunzi wake wakamjia.
2
Ndipo akaanza kuwafundisha, akisema:
3
“Heri walio maskini wa roho, maana Ufalme wa Mbinguni ni wao.
4
Heri wale wanaohuzunika, maana hao watafarijiwa.
5
Heri walio wapole, maana hao watairithi nchi.