Mathayo 27:6-10
6
Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.”
7
Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni.
8
Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo.
9
Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli,
10
wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”
Settings