Skip to content
Mathayo 27:6-10

Mathayo 27:6-10

6
Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.”
7
Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni.
8
Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo.
9
Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli,
10
wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options