Mathayo 26:48-50
48
Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
49
Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
50
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.