Skip to content
Mathayo 26:39-44

Mathayo 26:39-44

39
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
40
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
41
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
42
Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
43
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
44
Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options