Mathayo 24:32-35
32
“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yote, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
34
Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
35
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Settings