Skip to content
Mathayo 23:1-7

Mathayo 23:1-7

1
Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake:
2
“Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose,
3
hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri.
4
Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.
5
“Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao.
6
Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi.
7
Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options