Skip to content
Mathayo 17:1-8

Mathayo 17:1-8

1
Siku sita baada ya jambo hili, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana ndugu yake Yakobo, akawapeleka juu ya mlima mrefu peke yao.
2
Wakiwa huko, Yesu alibadilika sura mbele yao. Uso wake ukangʼaa kama jua na nguo zake zikawa na weupe wa kuumiza macho.
3
Ghafula wakawatokea mbele yao Mose na Eliya, wakizungumza na Yesu.
4
Ndipo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vyema sisi tukae hapa. Ukitaka, nitafanya vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
5
Petro alipokuwa angali ananena, ghafula wingu lililongʼaa likawafunika, na sauti ikatoka kwenye hilo wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana. Msikieni yeye.”
6
Wanafunzi waliposikia haya, wakaanguka chini kifudifudi, wakajawa na hofu.
7
Lakini Yesu akaja na kuwagusa, akawaambia, “Inukeni na wala msiogope.”
8
Walipoinua macho yao, hawakumwona mtu mwingine yeyote isipokuwa Yesu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options