Skip to content
Mathayo 15:1-9

Mathayo 15:1-9

1
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
2
“Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
3
Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4
Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
5
Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
6
basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
7
Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
8
“ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9
Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’ ”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options