Skip to content
Mathayo 13:53-58

Mathayo 13:53-58

53
Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
54
Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
55
“Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56
Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
57
Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
58
Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options