Skip to content
Marko 9:43-48

Marko 9:43-48

43
Kama mkono wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili lakini ukaingia jehanamu, mahali ambako moto hauzimiki. [
44
Mahali ambako funza wake hawafi wala moto wake hauzimiki.]
45
Kama mguu wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili lakini ukaingia jehanamu. [
46
Mahali ambako funza wake hawafi wala moto hauzimiki.]
47
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe. Ni afadhali kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa jehanamu,
48
mahali ambako “ ‘funza wake hawafi, wala moto wake hauzimiki.’
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options