Marko 10:5-9
5
Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6
Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
7
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
8
Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
9
Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
Settings