Skip to content
Luka 22:39-42

Luka 22:39-42

39
Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
40
Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
41
Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
42
akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options