Luka 21:29-33
29
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Settings